Psalms 20

Maombi Kwa Ajili Ya Ushindi

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi)


1 a Bwana na akujibu unapokuwa katika dhiki,
jina la Mungu wa Yakobo na liwe kinga yako.

2 bNa akutumie msaada kutoka patakatifu
na akupatie msaada kutoka Sayuni.

3 cNa azikumbuke dhabihu zako zote,
na azikubali sadaka zako za kuteketezwa.

4 dNa akujalie haja ya moyo wako,
na aifanikishe mipango yako yote.

5 eTutashangilia kwa furaha utakaposhinda,
tutainua bendera zetu kwa jina la Mungu wetu.
Bwana na akupe haja zako zote.


6 fSasa nafahamu kuwa Bwana
humwokoa mpakwa mafuta wake,
humjibu kutoka mbingu yake takatifu
kwa nguvu za wokovu wa mkono wake wa kuume.

7 gWengine wanatumaini magari ya vita, na wengine farasi,
bali sisi tutalitumainia jina la Bwana, Mungu wetu.

8 hWao wameshushwa chini na kuanguka,
bali sisi tunainuka na kusimama imara.


9 iEe Bwana, mwokoe mfalme!
Tujibu tunapokuita!
Copyright information for SwhKC